Sunday, December 7, 2008

EVE NDANI YA BONGO

Mwanamziki kutoka Marekani Jehan Jeffers a.k.a EVE akiongozana na mwenyeji wake Joseph Kusaga mara baada ya kuwasili TZ.Vilevile mwanamziki Fat Joe anategemewa kuwasili usiku wa leo.

EID MUBARAK WADAU!





Wadau weekend


Friday, December 5, 2008

Thursday, December 4, 2008

Mengi adai waziri ataka kumuhujumu..

TAARIFA YA BW. REGINALD A. MENGI, MWENYEKITI MTENDAJI WA IPP LIMITED KWA VYOMBO VYA HABARI.

Hivi karibuni waziri mmoja kijana anayeongoza wizara nyeti alipendekeza nibambikiziwe kodi bandia ya kiasi kikubwa nitakachoshindwa kulipa na hatimaye nifilisiwe kama njia pekee ya kuninyamazisha kabisa eti kama alivyofilisiwa tajiri mmoja mkubwa huko Urusi.

Alidai kwamba vyombo vyangu vya habari vimekuwa mno mstari wa mbele kupiga vita ufisadi, jambo ambalo kwa maoni yake siyo zuri kwa sababu linawanyanyasa baadhi ya watu.

Nilitegemea waziri huyo msomi sana angefahamu jinsi vyombo vya habari vinavyofanya kazi. Angalao angefahamu kwamba anayeamua nini kiandikwe na nini kisiandikwe ni mhariri wa gazeti ambaye taaluma yake ni uandishi wa habari na siyo mmiliki wa vyombo vya habari.Kama mkiristo na kama alivyoagiza Bwana Yesu namsamehe kwa vile hajui atendalo.

Baada ya kumsamehe ningetaka ajue yafuatayo.Asiyekemea maovu katika jamii, yeye ni sehemu ya maovu hayo. Waziri huyu na wale wote ambao wamekwishanitumia vitisho wakumbuke kwamba hata kama watafanikiwa kuvinyamazisha kwa hujuma zozote zile, vyombo vyangu vya habari, na hata kama mimi sitakuwepo tena, moto wa kupiga vita ufisadi uliokwishawashwa katika akili za wanajamii hauwezi kuzimika kamwe.

Ieleweke pia kwamba sauti za maskini na wanyonge katika jamii hazisikiki kwa urahisi. Vyombo vya habari husaidia kupaaza sauti na vilio vyao katika vita dhidi ya maovu. Ni wajibu wa kila mtu aliye na uwezo kusema kwa sauti kubwa kwa niaba ya wanyonge na maskini ili kutokomeza ufisadi.

Nachukua fursa hii kumpongeza sana Rais wetu Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuguswa na sauti na vilio vya wanyonge na maskini wa Tanzania kuhusu ufisadi na hatua za kijasiri zinazochukuliwa na Serikali yake dhidi ya ufisadi.

Sisi sote ni lazima tuzidi kumwomba Mwenyezi Mungu azidi kumpa ujasiri, nguvu na hekima nyingi wakati huu wa majaribio makubwa.

Wednesday, December 3, 2008

JOE THOMAS, Tanto Metro & Devonte Watua




Wasanii wa Kimataifa, Joe Thomas na Danto Metro & Devonte wametua Dar jioni hii tayari kwa shoo ya muziki ya Lykizo Time Ijumaa ijayo itakayofanyika Leaders Club.

ITS SO FUNNY!!

Mugabe was sitting with Tsvangirayi and Mutambara in Saudi Arabia , sharing a smuggled barrel of beer, when all of a sudden the police entered and arrested them.
They were initially given a death sentence but, as it was a national holiday, the sheikh decided they shouldbe released after each receiving 20 lashes of the whip.
As they were preparing for their punishment, the sheikh said, "It's my first wife's birthday today and she asked me to allow each of you one wish before your whipping, but you cannot wish not to be whipped!"
Mutambara thought for a second then said: "Please tie a pillow to my back before whipping." This was done but the pillow lasted 10 lashes.
Mugabe saw this and said: "Please tie two pillows to my back before whipping." This was done and lasted for the whole 20 lashes.
Tsvangirayi saw this, but before he could make his wish, the sheikh said: "As you are from the most popular party of Zimbabwe with all the wealth and you share the same ethnicity with Barack Obama, you are permitted to have two wishes!"
Tsvangirayi thought for a second, then said:"Thank you, most royal and merciful highness. My first wish is to receive 100 lashes with the strongest, toughest whip available."
"If you so desire," the sheikh replied with a questioning look on his face, "and your second wish?"
Tsvangirayi replied
"Tie Mugabe to my back."