Tuesday, December 30, 2008

HAPPY NEW YEAR!!


May all the dreams in your eyes, all the desires in your heart and all the hopes in your life blend together, to give you the most spectacular New Year ever. Happy New Year!!!!!

Tuesday, December 23, 2008

MAHARAGE: Chakula bora kwa wenye presha, kisukari
BAADHI ya watu hawapendi kutumia maharage kama mboga kutokana na kuonekana kama ni mboga ya kimasikini, lakini kiafya maharage ni miongoni mwa mboga zenye faida kubwa mwilini na hutoa ahueni kubwa kwa watu wenye matatizo mbalimbali ya kiafya kama tutakavyoona leo katika makala haya;
Kwa mujibu wa utafiti mbalimbali, maharage, hasa yale meusi, ni chanzo kizuri cha kirutubisho aina ya ‘faiba’ kinachoshusha kiwango cha kolestro mwilini. Vile vile kiwango cha ‘faiba’ kilichomo kwenye maharage meusi, huweza kudhibiti kiwango cha sukari kisipande haraka baada ya chakula, hivyo kufanya maharage kuwa lishe nzuri kwa wagonjwa wa kisukari na shinikizo la juu la damu.
Iwapo utapata mchanganyiko wa maharage meusi na ule mchele ‘mweusi’ ambao haujakobolewa na kuondolewa virutubisho vyake muhimu (brown rice), basi utaweza kupata kiasi kikubwa cha protini na faiba ambacho huwezi kupata kutoka katika chakula kingine.
Aidha, utafiti wa muda mrefu uliofanywa na jarida moja lijulikanalo kama ‘Journal of Agriculture and Food Chemistry’, unaonesha kuwa mbali ya maharage kuwa na kiwango kikubwa cha ‘faiba’, pia maharage yana virubisho vingine vinavyojulikana kama ‘anthocyanins’ ambavyo hutoa kinga mwilini (antioxidant). Kiwango cha virutubisho hivyo kilichomo kwemye maharage, kinaelezwa kuwa ni kikubwa kuliko hata kinachopatikana kwenye matunda kama zabibu ambayo inaaminika kuwa na kiwango kikubwa zaidi.
Inaelezwa pia kuwa, watafiti walipofanya tathmini ya ziada kwenye maharage, waliweza kubaini kuwa maharage yanapokuwa meusi zaidi, ndivyo ambavyo kiwango kikubwa cha kinga kinavyoweza kupatikana, yakifuatiwa na maharage ya rangi nyekundu, kahawia, njano na mwisho meupe. Hii ina maana kwamba maharage meusi ndiyo yana virutubisho vingi zaidi kuliko maharage meupe na rangi nyingine.
Kwa ujumla, kiwango cha kinga (antioxidant) kilichomo kwenye maharage meusi ni mara kumi ya kile kinachopatikana kwenye matunda kama machungwa, zabibu na mengine. Hivyo unapokula maharage, siyo tu unapata ‘faiba’ ya kutosha bali pia unapata virutubisho muhimu mwilini kwa ajili ya kutengeneza kinga ya mwili dhidi ya vinyelezi vya maradhi.
Yafuatayo ni baadhi ya matatizo ya kiafya yanayoweza kudhibitiwa kwa kiasi kikubwa na ulaji wa maharage meusi kama ilivyothibitika katika tafiti mbalimbali za kisayansi;
MAHARAGE YANA KINGA DHIDI YA SARATANI Utafiti umefanyika na kuthibitisha kuwa maharage meusi yana uwezo wa kutoa kinga mwilini dhidi ya saratani za aina mbalimbali.
MAHARAGE KINGA DHIDI YA UGONJWA WA MOYO Utafiti ulionesha pia watu wanaokula chakula chenye kiwango kingi cha ‘faiba’ kama vile maharage, hawako hatarini kupatwa na magonjwa ya moyo, ikiwemo kiharusi.
MAHARAGE HUONGEZA NGUVU MWILINI Ulaji wa maharage meusi husaidia kurejesha madini chuma mwilini na hivyo kuupatia mwili wako nguvu.
MAHARAGE YANA PROTINI NYINGI Maharage yana kiwango cha juu cha protini bora mwilini, hivyo badala ya nyama nyekundu, ambayo ikizidi ina madhara mwilini, kula maharage meusi.
Hizo ndiyo faida za maharage mwilini ambazo kila mtu anapaswa kuzijua kwa faida ya afya yake ya sasa na ya baadae.

Monday, December 22, 2008

MARRY CHRISTMASS TO YOU ALL!!



God is Love
Christmas is all about love
Christmas is thus about God and Love
Love is the key to peace among all mankind
Love is the key to peace and happiness within all creation
Love needs to be practiced - love needs to flow - love needs to make happy
Love starts with your partner, children and family and expands to all world
God bless all mankind

Saturday, December 20, 2008

VIJUE VYAKULA VINAVYOZUIA KUZEEKA
Katika toleo lake la hivi karibuni, jarida linalojishughulisha na uandishi wa habari mbalimbali za masuala ya lishe, Eating Well Magazine, limetoa matokeo ya utafiti mbalimbali wa vyakula vinavyochelewesha kasi ya mtu kuzeeka haraka, (anti aging foods) kama ifuatavyo:

CHOKOLETI Katika kisiwa kimoja cha San Blas kilichopo Panama Marekani ya Kusini, kuna jamii moja ya watu wa Kuna ambao hawana matatizo ya magonjwa ya moyo ukilinganisha na wenzao wa Panama upande wa bara ambao wanasumbuliwa na maradhi ya moyo mara tisa zaidi ya wenzao!
Sababu ya jamii moja kuwa salama kiasi hicho ni kutokana na kupenda sana kunywa kwa wingi vinywaji vitokanavyo na zao la kakao (cocoa) ambalo lina kiwango kikubwa cha kirutubisho aina ‘flavanols’ ambacho kina uwezo wa kuimarisha utendaji kazi wa mishipa ya damu (blood vessels). Inaelezwa kuwa uimarishaji wa mishipa ya damu, hupunguza hatari ya mtu kupatwa na ugonjwa wa kisukari, magonjwa ya figo na magonjwa ya akili.

SAMAKI Miaka 30 iliyopita, watafiti wa masuala ya lishe na magonjwa, walianza kufanya utafiti wa kujua kwa nini jamii ya watu wa Inuits waliyoko Alaska walikuwa hawasumbuliwi na ugonjwa wa moyo kabisa. Katika utafiti wao, walikuja kugundua kuwa jamii hiyo inakula idadi kubwa sana ya samaki ambao wana kirutubisho cha ‘Omega-3’ kinachozuia kujijenga kwa kolestro mwilini na kuimarisha mapigo ya moyo kuwa sawa.
KARANGAUtafiti uliowahi kufanywa na madhehebu ya Wasabato, ambao husisitiza ulaji unaozingatia afya na lishe ya mboga za majani (vegetarian), unasema kuwa mtu anapokula karanga, huongeza wastani wa miaka miwili na nusu katika umri wake wa kuishi. Karanga ni chanzo kikubwa cha mafuta asili, hivyo hutoa faida sawa na zile zinopatikana kwenye Olive Oil. Pia karanga ina kiwango kikubwa cha vitamini, madini na virutubisho vingine, vikiwemo vya kukinga mwili.

MVINYO (WINE) Utafiti unaonesha kuwa unywaji wa kilevi kwa kiwango cha kawaida, hutoa kinga dhidi ya magonjwa ya moyo, kisukari na upotevu wa kumbukumbu kichwani kutokana na umri mkubwa. Kwa mujibu wa utafiti huo, aina mbalimbali za vileo (alcohol) zinaonesha kuwa na faida hizo, lakini mkazo wa utafiti umeelekezwa zaidi kwenye mvinyo mwekundu. Inaelezwa kuwa mvinyo mwekundu una kirutubisho kiitwacho ’resveratrol’ ambacho, kwa mujibu wa utafiti, huzuia kuzeeka kwa chembechembe za mwili.

MTINDI Mwaka 1970, Georgia ya Urusi, ilidaiwa kuwa na idadi kubwa ya wazee wenye umri wa miaka 100 kuliko nchini nyingine duniani. Taarifa za wakati huo, zilidai kuwa siri ya watu wengi kuwa na umri mkubwa kama huo ni mtindi, ambao huliwa katika mlo wao wa kila siku. Wakati uwezo wa mtindi kurefusha maisha ya mtu haujathibitishwa kisayansi, lakini inaeleweka kuwa mtinmdi una kiasi kikubwa cha madini ya kashiamu na aina fulani ya ‘bacteria’ ambao hutoa kinga kwenye utumbo mdogo dhidi ya maradhi mbalimbali ya tumbo.
Mwisho, kumbuka kuwa jinsi ulivyo au utakavyokuwa baadaye, kunatokana na unavyokula, hivyo jitahidi kuwa ‘mchaguzi’ kwa kila kitu unachokula ili kulinda afya yako.

Friday, December 19, 2008

WAANDAMANA KUPINGA UUAJI WA PAKA KWA AJILI YA CHAKULA


Polisi wakiwanyang'anya raia picha zinazoonyesha paka waliokuwa-trapped kwa ajili ya kutengenezwa kitoweo.Hii ni Beijing tarehe 18 Desemba mwaka huu

Mmoja wa waandamanaji akiwa na picha ya paka waliofungiwa
Mmoja wa waandamanaji akilia kupinga matumizi ya paka kwa ajili ya chakula Beijing.


Monday, December 15, 2008

BUSH ARUSHIWA KIATU IRAQ!



Mwandishi wa habari akimrushia kiatu raisi G.W.BUSH wa marekani alipokuwa ziarani IRAQ.Jamaa alifanya ziara ya kushtukiza kwa ajili ya kuaga kabla ya kumaliza muda wake mapema january.

Saturday, December 13, 2008

MAMBO YA RUGBY!!



ANUSURIKA KIFO BAADA YA KUCHOMWA NA MSHALE KICHWANI!!


Mwanafunzi wa umri wa miaka 11 nchini China (pichani juu), amenusurika kufa baada ya mshale uliorushwa na rafiki yake kuzama kichwani mwake kupitia kwenye jicholake, aliwahishwa hospitali huku mshale huo ukiwa bado umezama kwenyekichwa chake...kwa habari zaidi: NIFAHAMISHE.COM



Source; www.abdallahmrisho.blogspot.com






HABARI NJEMA

Kwa watu mliopo mbali na Tanzania,taarifa za habari kutoka Radio One,Radio Free Africa,Radio Uhuru na TBC zaweza kupatikana through www.dullonet.com

UMUHIMU WA NDIZI MBIVU KWENYE AFYA YAKO

Baada ya kusoma makala yangu ya leo na kuzingatia nilichokiandika, bila shaka utaanza kuingalia ndizi kwa mtizamo tofauti na uliokuwa nao hapo awali। Ndizi mbivu ni tunda maarufu sana duniani lakini ni watu wachache wanaojua uwezo, faida na maajabu yaliyomo kwenye tunda hili।Ndizi ina aina tatu za kipikee za sukari zinazojulikana kitaalamu kama Sucrose, Fructose na Glucose na vile vile ina kiasi kingi cha ufumwele (fibre) ambacho husaidia sana katika usagaji wa chakula tumboni.Ndizi ina uwezo mkubwa wa kuongeza na kuimarisha nishati ya mwili. Unaweza kupata nishati ya kufanyakazi ya muda wa dakika 90 kwa kula ndizi mbili tu. Bila shaka ndizi ni tunda muhimu sana kwa wanamichezo. Hata hivyo, nishati siyo faida pekee unayoweza kuipata katika ndizi, ni tunda lenye uwezo pia wa kuponya na kuzuia matatizo mengi ya kiafya:MFAIDHAIKO WA AKILI (DEPRESSION)Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Chama Cha Afya ya Akili cha Taifa (MIND) cha nchini Uingereza, kwa watu wanaosumbuliwa na tatizo la mfadhaiko wa akili, watu wengi waliondokana na tataizo hilo na kujisikia vizuri baada ya kula ndizi mbivu. Hali hii inatokana na ukweli kwamba ndizi ina kirutubisho kinachojulikana kama tryptophan, ambacho ni aina fulani ya protini inayotumika mwilini kumfanya mtu kuwa mtulivu na mwenye furaha.MATATIZO WAKATI WA HEDHI (PMS)Kama wewe ni miongoni mwa wale akina mama wanaopatwa na matatizo mbalimbali ya kiafya wakati wa hedhi, unashauriwa kula ndizi mbivu na unaweza kuponywa. Vitamin B6 iliyomo kwenye ndizi, hurekebisha kiwango cha sukari ambacho huweza kuathiri hali ya mtu.UPUNGUFU WA DAMU (ANAEMIA)Ndizi ikiwa ni chanzo kizuri cha madini aina ya chuma (iron), inaweza kuwa ni dawa ya kuzuia na kuponya upunguvu wa damu kwa sababu madini ya chuma huamsha uzalishaji wa chembechembe za damu mwilini.SHINIKIZO LA DAMUTunda hili ni la aina ya kipekee, lina kiwango kikubwa cha madini ya potasiamu (potassium) na wakati huo huo lina kiasi kidogo sana cha chumvi (sodium) hivyo kulifanya kuwa tunda bora katika kupambana na tatizo la kupanda na kushuka kwa shinikizo la damu.Ukweli huo, hivi karibuni umeifanya Mamlaka ya Dawa na Chakula ya nchini Marekani, iwaruhusu wazalishaji na wauzaji wakubwa wa ndizi nchini humo, kutangaza rasmi uwezo wa ndizi katika kupambana na hatari ya shinikizo la damu na kupatwa na kiharusi (stroke) kwa binadamu.NGUVU YA AKILIHivi karibuni, wanafunzi wapatao 200 wa Shule ya Twickenham nchini Uingereza, walisaidiwa kufaulu mitihani yao kwa kula ndizi mbivu wakati wa mlo wa asubuhi (breakfast), wakati wa mapumziko na wakati wa chakula cha mchana, ndizi ziliongeza uwezo wa akili zao. Utafiti unaonesha kuwa potasiamu iliyojazana kwenye ndizi, ina uwezo wa kumsaidia mwanafunzi kuamsha uwezo wake wa kujisomea.KASUMBA (HANGOVERS)Moja ya dawa ya haraka ya kuondoa uchovu unaotokana na ulevi wa jana yake (hangover) ni kunywa ‘Milkshake’ iliyotengenezwa kwa ndizi na kutiwa asali. Ndizi hutuliza tumbo, ikisaidiwa na asali, hurejesha kiwango cha sukari kilichopungua kwenye damu wakati maziwa hutuliza na kurejesha maji kwenye mfumo wake.Mbali na matatizo yaliyoelezwa hapo juu, ndizi pia husaidia katika matatizo mengine mengi kama vile kutuliza mishipa ya fahamu, kuondoa wasiwasi, kutuliza vidonda vya tumbo, kuondoa asidi tumboni, kushusha joto mwilini, kurekebisha mapigo ya moyo, n.kHivyo ndizi ni tiba ya magonjwa mengi na ni bora, ukiilinganisha na Epo (Apple), ndizi ina protini mara nne zaidi, wanga mara mbili, vitamin A na chuma mara tano na vitamini na madini mengine mara mbili zaidi ya epo. Mwisho; USIWEKE NDIZI KWENYE JOKOFU!

Sunday, December 7, 2008

EVE NDANI YA BONGO

Mwanamziki kutoka Marekani Jehan Jeffers a.k.a EVE akiongozana na mwenyeji wake Joseph Kusaga mara baada ya kuwasili TZ.Vilevile mwanamziki Fat Joe anategemewa kuwasili usiku wa leo.

EID MUBARAK WADAU!





Wadau weekend


Friday, December 5, 2008

Thursday, December 4, 2008

Mengi adai waziri ataka kumuhujumu..

TAARIFA YA BW. REGINALD A. MENGI, MWENYEKITI MTENDAJI WA IPP LIMITED KWA VYOMBO VYA HABARI.

Hivi karibuni waziri mmoja kijana anayeongoza wizara nyeti alipendekeza nibambikiziwe kodi bandia ya kiasi kikubwa nitakachoshindwa kulipa na hatimaye nifilisiwe kama njia pekee ya kuninyamazisha kabisa eti kama alivyofilisiwa tajiri mmoja mkubwa huko Urusi.

Alidai kwamba vyombo vyangu vya habari vimekuwa mno mstari wa mbele kupiga vita ufisadi, jambo ambalo kwa maoni yake siyo zuri kwa sababu linawanyanyasa baadhi ya watu.

Nilitegemea waziri huyo msomi sana angefahamu jinsi vyombo vya habari vinavyofanya kazi. Angalao angefahamu kwamba anayeamua nini kiandikwe na nini kisiandikwe ni mhariri wa gazeti ambaye taaluma yake ni uandishi wa habari na siyo mmiliki wa vyombo vya habari.Kama mkiristo na kama alivyoagiza Bwana Yesu namsamehe kwa vile hajui atendalo.

Baada ya kumsamehe ningetaka ajue yafuatayo.Asiyekemea maovu katika jamii, yeye ni sehemu ya maovu hayo. Waziri huyu na wale wote ambao wamekwishanitumia vitisho wakumbuke kwamba hata kama watafanikiwa kuvinyamazisha kwa hujuma zozote zile, vyombo vyangu vya habari, na hata kama mimi sitakuwepo tena, moto wa kupiga vita ufisadi uliokwishawashwa katika akili za wanajamii hauwezi kuzimika kamwe.

Ieleweke pia kwamba sauti za maskini na wanyonge katika jamii hazisikiki kwa urahisi. Vyombo vya habari husaidia kupaaza sauti na vilio vyao katika vita dhidi ya maovu. Ni wajibu wa kila mtu aliye na uwezo kusema kwa sauti kubwa kwa niaba ya wanyonge na maskini ili kutokomeza ufisadi.

Nachukua fursa hii kumpongeza sana Rais wetu Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuguswa na sauti na vilio vya wanyonge na maskini wa Tanzania kuhusu ufisadi na hatua za kijasiri zinazochukuliwa na Serikali yake dhidi ya ufisadi.

Sisi sote ni lazima tuzidi kumwomba Mwenyezi Mungu azidi kumpa ujasiri, nguvu na hekima nyingi wakati huu wa majaribio makubwa.

Wednesday, December 3, 2008

JOE THOMAS, Tanto Metro & Devonte Watua




Wasanii wa Kimataifa, Joe Thomas na Danto Metro & Devonte wametua Dar jioni hii tayari kwa shoo ya muziki ya Lykizo Time Ijumaa ijayo itakayofanyika Leaders Club.

ITS SO FUNNY!!

Mugabe was sitting with Tsvangirayi and Mutambara in Saudi Arabia , sharing a smuggled barrel of beer, when all of a sudden the police entered and arrested them.
They were initially given a death sentence but, as it was a national holiday, the sheikh decided they shouldbe released after each receiving 20 lashes of the whip.
As they were preparing for their punishment, the sheikh said, "It's my first wife's birthday today and she asked me to allow each of you one wish before your whipping, but you cannot wish not to be whipped!"
Mutambara thought for a second then said: "Please tie a pillow to my back before whipping." This was done but the pillow lasted 10 lashes.
Mugabe saw this and said: "Please tie two pillows to my back before whipping." This was done and lasted for the whole 20 lashes.
Tsvangirayi saw this, but before he could make his wish, the sheikh said: "As you are from the most popular party of Zimbabwe with all the wealth and you share the same ethnicity with Barack Obama, you are permitted to have two wishes!"
Tsvangirayi thought for a second, then said:"Thank you, most royal and merciful highness. My first wish is to receive 100 lashes with the strongest, toughest whip available."
"If you so desire," the sheikh replied with a questioning look on his face, "and your second wish?"
Tsvangirayi replied
"Tie Mugabe to my back."

Tuesday, December 2, 2008

MAMBO YA KP



HATIMAYE JAMAA WAPATA ZALI LA DHAMANA

photos
[/b]MAFISADI WAPATA DHAMANA
Hatimaye Mramba na Yona wamepewa dhamana na mahakama ya Kisutu ya jijini Dar es Salaam baada ya kuwasilisha hati za mali walizonazo na kukubaliwa na Hakimu Mkazi Ezron Mwankenja.

Mramba amewasilisha hati nne zenye jumla ya shingi Bilioni 3.1 na Yona aliwasilisha hati 3 zenye jumla ya shilingi Bilioni 2.6.Je watanzania tunachezewa filamu au ndo hali halisi?

Monday, December 1, 2008

Disemba mosi


siku ya ukimwi disemba mosi
wadau tuliikumbuka siku hii??

Aliyekatika mikono akamatwa akinyonga usukani kwa miguu


Polisi mjini Beijing China, walipigwa na butwaa baada ya kukuta dereva waliyemsimamisha hana mikono na alikuwa akinyonga usukani kwa kutumia miguu...
kwa full news nenda NIFAHAMISHE.COM

Mambo ya KP

5 Ways to Protect Yourself from the Flu

There are few steps that you can take to protect yourself and your family from what seems to be the inevitable flu. The guardian of the health of our body is the immune system. While intangible and challenging to identify, the immune system has very specific signs and symptoms.

I’d like you to consider some new approaches and angles that will provide you with insight into the likelihood that you will stay healthy or get sick this winter season.

1. Sugar and processed foods impact the immune system.

Studies have shown that through a complex system of chemical processes sugar and processed foods depress the immune system. There exists a direct link between the amount of these foods that your child consumes and his/her health.

Obvious foods such as sodas, candy, cookies, ice cream, and potato chips are the big guns that should be kept concealed.

Even more disturbing are the foods that you think are healthy for your child that hide sugar and many refined ingredients: yogurt, and yogurt drinks and “pops;”most cereals; juices; fruit roll ups and “leathers;” “healthy” cookies and treats, soy ice cream and frozen treats. While being marketed as healthy choices, these foods aren’t much better than the obvious poor choices. Work hard during flu season to keep these foods away from your children. Read ingredient labels and watch out for: corn syrup, high fructose corn syrup or “HFCS,” brown rice syrup, fructose, sucrose, barleymalt and the obvious, sugar.

2. Fresh foods offer the highest quality vitamins.

It’s shocking to me how often I see people turn to orange juice for vitamin C in an effort to fight off a cold or flu.

It is important to understand that the majority of vitamin C in orange juice is added after processing. Vitamin C and others like zinc, vitamin E, and magnesium help to support the immune system and are a great defense during flu season.

Choose better by having kids eat fresh whole foods such as cherries, berries, and apples, and vegetables such as spinach, kale, Brussels sprouts, broccoli, carrots and sweet potatoes.

I know you probably hear this suggestion all the time, but it can’t be stressed enough. It is imperative to find creative ways to prepare vegetables so that kids will actually eat them. Sautee, roast or grill vegetables with olive oil or real butter, add some fresh sea salt or sprinkle with organic low fat cheese and kids will be more likely to eat.

3. Sleep will boost the immune system.

At night while we rest, the body is working to rebuild the immune system. Deep sleep allows a complex set of hormonal changes that recharge the body so that it’s resilient the next day. Be diligent and ensure that kids get a full night sleep of 8-10 hours.

Mandate bedtime despite protests and stick to a regular schedule. These are the times that mom and dad really need to be the boss. Resist the temptation to allow your child to stay up late and watch his or her favorite show. At the end of the day when you are tired as well, it’s easy to give in to your child’s vigilant campaign.

Remember: Would you rather avoid the confrontation tonight? Or deal with a sick kid tomorrow?

4. Fatigue is the first sign of a distressed immune system.

As already stated, the immune system desperately needs sleep to keep the body healthy. When the immune system is fighting to keep your child healthy, it requests that the body get extra rest to help in the fight.

If your child seems more fatigued than usual, it could be a very strong signal that your child is on the brink of getting sick.

The best way to fight off a cold or flu is to act immediately and get extra rest. Pay attention to the health of others around you such as those at work or your child’s school. If you hear of a bug “going around” and you notice that your child is tired, there’s a good chance that extra sleep will ward off the cold or flu. This is the time to allow extra television and require a mid-day nap.

5. Wash hands frequently, but avoid antibacterial products.

This seems counterintuitive, but the best way to kill environmental germs is to use soap and hot water and scrub hands thoroughly. Bacteria live all around us. They are on every surface we touch and in every breath we take. Without bacteria, our immune system wouldn’t learn to be strong.

Our internal bacterial system fights off invaders and thereby gets more effective at winning the battle. It’s just like working out: In order to become stronger, you must work hard in the gym. Your child’s body is a bacterial gym. Again, this comes back to the immune system. If you foster a strong immune system, your child’s body will fight off invaders and therefore become more resilient to future battles. While it is imperative to wash hands frequently during flu season, remember that the hands are only one very small way that germs enter your child’s system. Killing off the germs on hands with antibacterial products is futile and weakens your child’s- and the world’s- future ability to confront germs.
source; www.yahoo.com

Saturday, November 29, 2008

BLACK HISTORY SPOTLIGHT: DR. ALEXA CANADY

DR. ALEXA I. CANADY (1950-) is the first black female neurosurgeon.

Canady was born November 7, 1950, to Clinton and Elizabeth Canady. Her father was a dentist, and her mother served as president of Delta Sigma Theta sorority, in addition to other civic affairs. The family lived just outside Lansing, Michigan. Canady and her brother were the only two black students in their entire school.

Canady was an exceptional student and named a National Achievement Scholar in 1967. She attended the University of Michigan, earning her bachelor’s in zoology in 1971, although she had almost dropped out of college. She explains, “The summer after my junior year, I worked in Dr. Bloom’s lab in genetics and attended a genetic counseling clinic. I fell in love with medicine.”

She continued her studies at the University of Michigan Medical School, earning her M.D. in 1975, graduating cum laude. Following graduation, Canady interned at Yale’s New Haven Hospital for a year. She was appointed the first female and first black person to a residency in neurosurgery. On her first day, as she began making her rounds, a hospital administrator referred to her as “the new equal-opportunity package.” Despite the remark, Dr. Canady viewed her accomplishment as a double achievement for not only herself, but also her race and gender.

In 1976, Canady went to work at the University of Minnesota in its neurosurgery department until 1981. She then worked at the University of Pennsylvania Children’s Hospital in pediatric neurosurgery for a year. In 1982, she began working at the Children’s Hospital in Detroit, and in 1987, Canady became director of neurosurgery there. She held this position until her retirement in June 2001.

Despite her work load, Canady would make time when mentor programs asked her to take a high school student around for the day. In a Free Press interview, she explained, “I do it because it’s important. If you want to be something, you have to perceive that something is possible. You do a disservice to children if you paint it as too rosy. They hit a bump and feel like a failure. Well, everybody fails at some time or another. But no one talks about it.”

Dr. Canady holds two honorary degrees: a doctorate of humane letters from the University of Detroit-Mercy, awarded in 1997, and a doctor of science degree from the University of Southern Connecticut, awarded in 1999. She received the Children’s Hospital of Michigan’s Teacher of the Year award in 1984, and was inducted into the Michigan Woman’s Hall of Fame in 1989. In 1993, she received the American Medical Women’s Association President’s Award and in 1994 the Distinguished Service Award from Wayne State University Medical School. In 2002, the Detroit News named her Michiganer of the Year.

Now that she’s retired, Dr. Canady has more time to work to change the perspective of how blacks both as patients and physicians are being presumed and perceived. She claims the major medical problem for blacks stems from the scarcity of research targeting their specific health concerns and needs. She enjoys playing video games and having more time to spend with her husband, George Davis, a retired Navy recruiter.

Friday, November 28, 2008

Baada ya Obama Afrika kupata rais mweupe?



NELSON Mandela alikuwa Rais mweusi wa kwanza Afrika ya Kusini, na watu wote wapenda amani walifurahi na kuamini kuwa sasa ubaguzi wa rangi umekwisha na watu weusi ambao ni wengi watafaidi matunda ya harakati zao.

Walitarajia maisha bora kwa wote na uchumi wa nchi kuwanufaisha wote. Sisi pia tuliposaini mikataba ya ushirikiano wa kibiashara tulidhani tutaona weusi wengi wenye uwezo wa kifedha, elimu na viwanda watatusaidia sisi tuliojitoa mhanga kwa ajili yao.

Hatukujaliwa kukumbuka kuwa mfumo wa ukoloni mkongwe, ubepari na ubaguzi uliotawala nchi hiyo kwa miongo mingi haukuwa umemtayarisha mtu mweusi kushika hatamu za uchumi kwa hiyo siasa na jamii. Matokeo yake wengi wana uchungu wa kuona “kaburu” kahamia Tanzania na ana kula kuku kwa mrija kwa jina la ushirikiano wa kibiashara.

Leo hii watu weusi wa Afrika ya Kusini hawana tafauti na wenzao Kaskazini ya mto Limpopo ambao tulipata uhuru wa bendera tu.

Sasa tumepata Rais mweusi mwingine wa kwanza katika Marekani! Kwa vile fungate la ushindi huo limekwisha, inabidi tuanze kujiuliza maswali magumu: Je hii ina maana gani kwetu? Waamerika wenyewe wanajigamba kuwa uchaguzi huo ni mfano wa kiwango cha juu cha demokrasia popote.

Ni kweli, kama ambavyo Rais Bush ni Rais wa Marekani, na si Rais wa Marekani mwenye asili ya Ulaya, Obama naye anaitwa Rais mteule wa Marekani, na si Rais Mteule wa Marekani mwenye asili ya Afrika.

Kwa hiyo, kisaikolojia mtu mweusi kapanda hadhi kidogo kwa kutambuliwa kuwa ni raia kamili wa Marekani.

Ila kwa nini iwe hivyo sasa? Ni kweli kwamba demokrasia ya Marekani imekomaa hasa wakati huu inapojenga himaya yake duniani kote au kuna jingine? Nini athari ya demokrasia ya Marekani kwa Afrika?

Kwa tathmini yangu, hasa nikiangalia miaka kadhaa ijayo naona kuna ajenda. Kwanza ni ile dhana ya utandawizi kwamba dunia sasa ni kijiji kimoja na ye yote mwenye nia, ari, uwezo anaweza akawekeza popote na hata kutawala katika nchi kama Marekani!


Obama
Obama

Obama, ambaye babake ni Mkenya lakini yeye ni Mmarekani, ameweza kufanikiwa kupata cheo kikubwa duniani, tena akiwa na umri mdogo kabisa. Kwa maana hiyo, wapo weupe wengi waliozaliwa na kukulia Afrika; yaani Wazungu, Waarabu, Wahindi, Wachina na wengine. Kwa sasa tunao marais weupe Afrika, lakini wanaishia katika nchi za Afrika ya Kaskazini.

Tukifuata demokrasia ya Marekani ni kwamba kuna siku bara la Afrika litapata marais wengi weupe. Na hawa wataiunganisha Afrika ili ipate Rais mmoja.

Naweza nikaonekana naota ndoto ya alinacha; lakini kwa jinsi dunia inavyokwenda, suala hili si ndoto.

Kwa mfano tukishindwa kulipa madeni na kutangazwa mufilisi, mweupe mmoja kama Bill Gates au Mfalme wa nchi za Kiarabu anaweza akatununua kwenye mnada tu! Wakubwa wanajua Waafirka hatujawahi kuwatawala na kuwanyanyasa mataifa mengine katika nchi zao, kwa hiyo ni rahisi kwa mtwana kuwa “bwana”. Lakini wao kuja kututawala sisi huo utakuwa ni ukoloni au utumwa kujirudia!

Kuna wanao dai kwamba Obama ni kizazi kipya cha Waafrika, kwa vile baba yake hakutokana na kizazi kilichochukuliwa utumwa. Ukweli unabaki palepale: hizo ni propaganda za kutugawa ili wengine wajione bora kuliko wengine. Mtu mweusi popote duniani ni taifa lililonyanyaswa kuliko yote katika historia, na wote ni waathirika na waadhirika wa biashara dhalimu ya utumwa hadi leo!

Hebu fikiria Afrika ya Kusini au Kenya ipate Rais mweupe leo, itawezekana? Ilichukua karne nyingi kwa ngozi nyeusi kukubalika huko Marekani, lakini kwa ajili ya tabia yetu ya kusahau haraka itachukua muda mfupi kujiona sie tunakubalika sasa.

Na kwa vile hilo linajulikana na wakubwa, ndio maana zinatafutwa njia za mkato kama Obama, au pengine baadae Serikali ya Obama inaweza kuweka mkwara kutubana; tuwe na kipengele katika sheria za uchaguzi kisichobagua mtu kwa rangi yake kugombea nafasi kubwa kama urais kama tuna taka msaada.

Naamini kwa dhati raia wa Marekani waliopiga kura katika Uchaguzi wao mkuu uliopita walipigia kura mabadiliko. Waliamini serikali itakayoongozwa na chama cha Democrats, chini ya uongozi wa Rais mteule Obama, iko katika nafasi nzuri ya kuleta mabadiliko yanayotakiwa na wengi.

Swali kubwa ninalojiuliza: Obama ameweka wazi kwamba yeye ni Mmarekani na maslahi ya nchi yake yanakuja kwanza; je kuna tafauti gani kati ya Democrats na Republicans?

Kimsingi vyama hivi vikubwa Marekani vyote vinaweka maslahi ya Marekani kwanza, tafauti yao ni katika mbinu za utekelezaji. Naweza kufananisha Republicans na simba anaenguruma na kuonekana kwa urahisi na kutisha. Democrats ni nyoka ambaye huwezi kujua kwa urahisi kama yupo mpaka akung’ate.

Mbinu za Republicans ni za kibabe kama zile za polisi anayekupa mikong’oto ili umpe taarifa anayoitaka, ukiwa karibu kufa anakuja polisi mwema ambaye ni Democrat na kukwambia bora uongee na yeye!

Huyu (Democrat) anakuja kwa upole na kirafiki na maji atakupa na kusema yule jamaa hana msalie Mtume, bora umweleze yeye kila kitu; kisha yeye atajua namna ya kukusaidia. Kwa hiyo wakati Republicans wanatumia nguvu na ubabe, Democrats wanatumia diplomasia, lakini lengo linabaki palepale - maslahi ya kwanza ni kwa Marekani .

Je ni nani wanaamua na kudhibiti maslahi ya nchi? Katika kitabu chake “The secret history of the American Empire”, toleo la 2007, mwandishi John Perkins anasema: “Hawa wanaume na wanawake (waumini wa utawala unaoongozwa na wafanyi biashara wakubwa anao waita corporatocracy) ndio wanaoongoza nchi, hawajali ni chama gani kiko Ikulu au kina wabunge wengi bungeni.

Hawaguswi na matakwa ya umma, na hakuna sheria inayowapa kikomo cha kuongoza.” Na ndio wanaojenga Himaya ya Marekani, The Empire, yaani taifa kubwa kiuchumi, kijeshi na kisiasa.

Kwa nini walimwengu wanaifananisha Marekani na himaya kama zile za Warumi, Waingereza na wengine?

John Perkins ni Mmarekani ambaye alitumikia shirika la kimataifa lililotoa ushauri wa kupotosha uchumi wa nchi “masikini” za Asia, Marekani ya Kusini na Afrika kwa niaba ya himaya ya Marekani. Yeye na kundi la wataalamu wenzake walizishawishi nchi mbalimbali kukubali mikopo mikubwa kwa ajili ya maendeleo kama vile miradi mikubwa ya umeme, barabara, viwanja vya ndege, bandari na miji ya kisasa inayofanana na Marekani!

Kazi yao nyingine ilikuwa kuhakikisha kwamba mikataba ya miradi hiyo inaenda kwa kampuni za Kimarekani. Nchi hizi zikishaelemewa na madeni ndipo Serikali ya Marekani inakuja na mikakati ya kudai madeni kwa kutaka rasimali zenu au ushirikiano katika masuala ya kijeshi na siasa.

Matokeo yake ni nchi hizi kuendelea kufukarika na hivyo serikali kushindwa kutoa huduma muhimu kwa raia wake kwa vile inalipa madeni ambayo hayaishi; kwani yalikuwa ni mtego wa kifo.

Perkins anasema kwamba kama wao wakishindwa kuishawishi nchi ikubali kwa hiyari ya lazima, basi nchi hizi, ama huvamiwa kijeshi, au huyo kiongozi hupinduliwa na kibaraka kuingizwa madarakani.

Kwa sifa zake hizo na nyingine, Marekani inaitwa “Himaya” kwa vile ina vigezo vyote vya “Himaya”. Kwa mfano, kiu isiyoisha ya kutaka kutawala wengine na kunyonya rasilimali zao. Aidha ina ulafi wa rasilimali nyingi zaidi ukilinganisha na nchi zingine, na inakuwa na jeshi kubwa sana kuimarisha sera zake.

Hulka ya himaya yoyote kama Marekani ni kueneza lugha yake, fasihi, sanaa na utamaduni wake; hasa ule wa hovyo kwa makoloni yake. Huwatoza kodi hata watu ambao si raia wake katika nchi zingine. Hulazimisha kutumika sarafu na baadhi ya sheria zake kwa nchi zingine.

Perkins anasema kwamba Marekani ina sifa hizo zote. Kwa mfano, idadi ya watu wa Marekani ni asilimia tano (5%) ya watu wa dunia nzima, lakini inatumia zaidi ya asili mia ishirini na tano (25%) ya rasilimali za dunia nzima! Imefanikiwa katika hilo kwa kuzinyonya nchi zingine zenye uchumi unaokua.

Pamoja na kwamba himaya hii imejekengeka kwa njia za kiuchumi, lakini viongozi wote duniani wanajua njia zote zikishindikana jeshi lake kubwa na la kisasa litatumika. Kwenye himaya za zamani kulikuwa na watawala maalumu wakiitwa “Emperor” au Mfalme ambao hawakuchaguliwa kwa kura za watu wala hawakuwa na ukomo wa kutawala. Hawa walidhibiti serikali, jeshi na vyombo vya habari.

Marekani ina kundi la watu ambao wanatawala kwa pamoja mithili ya mfalme. Watu hao wanaendesha makampuni makubwa na kupitia hayo makampuni wanaendesha serikali, anasema John Perkins.

Na kwa vile wanafadhili kampeni za kisiasa na vyombo vya habari, wana uwezo mkubwa wa kuwadhibiti viongozi waliochaguliwa ikiwa ni pamoja na kuamua ni taarifa gani raia wazipate katika vyombo vya habari.

Ndio maana si ajabu Wamarekani wengi hawajui ukweli kuhusu nchi yao nje ya mipaka yao, na sisi hatujui mengi kuhusu Marekani; hata kama tunaangalia CNN saa zote!

Kwa kiasi kikubwa yaliyomo kwenye katiba ya Marekani - haki za watu na maneno mengi kuhusu demokrasia hayaendani na vitendo vyao wanapoangalia maslahi ya nchi yao.

Sasa hiyo ndio nchi ambayo Obama anatarajia kuiongoza baada ya kuapishwa rasmi! Sifa na heshima ya himaya hii iko chini na watu wengi duniani sasa wamechoshwa nayo; japo hawajui la kufanya.

Je Rais Mteule Obama ataweza kuleta mabadiliko ya sera za nje bila kuhatarisha maslahi ya himaya ya Marekani? Je huko ambako imeleta uharibifu, madhara na madhila, na watu wanajua ni kwa sababu ya sera za Marekani, atafanya nini?

Huku kwetu (Afrika) kwenye maliasili nyingi kama mafuta na madini na ukanda mkubwa wa bahari, kuna tishio la Marekani kuweka vituo vya kijeshi vya Africom. Je Obama ataendeleza mpango huo? Je Marekani, ambayo inatumia mabilioni ya mapesa, rasilimali watu na muda kutengeneza silaha za mauaji ya halaiki, itaweza kufunga na kuviteketeza viwanda vyake haramu na kutafuta njia mbadala ya kupata pesa? Rais Mteule Obama ataweza kupambana na watemi wa vita?

Rais Mteule atachwa atawale na kuongoza na kuleta mabadiliko au atatumiwa kama Afisa Uhusiano wakubadilisha taswira ya Marekani kwa walimwengu ?

Haya ni baadhi ya maswali tunayopaswa kujiuliza katika kipindi hiki ambacho Rais Mteule Obama anasubiri kuingia rasmi Ikulu ya Marekani kuanza kazi.

Article source;www.raiamwema.com

WEEKEND NJEMA

Mwaka 2008 upo mbioni kuelekea ukingoni mwake.Zimebaki wiki kadhaa tu kabla hatujaona zile fataki hewani na kusikia ving’ora vikitusindikiza kuumalizia mwaka.Kwa vyovyote vile mwaka 2008 utaenda na historia kadhaa zenyewe kuvutia kwa wengine na kutia simanzi kwa wengine.Ndio maisha.Ni mwaka ambao hakuna atakayeweza kamwe kusahau kwamba mtu mweusi wa kwanza amechaguliwa kuliongoza taifa kubwa la Marekani.

Lakini nchini kwetu pia ni mwaka ambao tunaweza kusema tumeshuhudia mengi ambayo siku za nyuma yalionekana kuwa hayawezekani.Tumeona viongozi kadhaa wakijiuzulu nyadhifa zao.Tumeshuhudia wengine wakipandishwa kwenye karandiga.Tumeona wazee wengine wakipandwa na pressure kwa sababu wanajua walishaharibu na hawana uhakika na kesho.Nadhani tunakubaliana kabisa kwamba miaka kadhaa ya nyuma,ilikuwa ni kama ndoto kusikia kiongozi akitangaza kujiuzulu.Mifano ya waliowahi kujiuzulu ilikuwa ni michache sana.

Inawezekana ni “changa la macho” na kwamba kinachofanyika ni mchezo wa aina yake wenye wingu zito la kisiasa.Inawezekana kabisa(hakuna lisilowezekana katika dunia hii).Lakini pamoja na yote hayo,tofauti na siku za nyuma,hata kile kitendo tu cha kuwaona waheshimiwa wakitokwa na jasho kwa sababu hawamo ndani ya yale “mashangingi” yao na badala yake wamekalia yale yale mabenchi ambayo hawakuwahi kuona umuhimu wa kuyakarabati kwa sababu “hayakuwahusu” na huku wakiwa wameegemea zile kuta ambazo hela yake ya rangi waliipeleka kusipotakiwa,ni vitu ambavyo vinaufanya mwaka 2008 uwe na lake katika historia.Bado tunasubiri kuona jinsi “changa la macho” litakavyopelekwa.Tupo na tunatizama kwa makini.Anayedhani tumelala anajidanganya.

Weekend njema!!

source-www.bongocelebity.com

Thursday, November 27, 2008

WAHESHIMIWA WANAPOWEKWA KITIMOTO



Inavutia kuona kwamba suala zima la jina la mtu haliangaliwi katika mkono wa sheria.
Waheshimiwa hawa(DANIEL YONA na BASIL MRAMBA) wakisomewa mashtaka yao katika mahakama ya Kisutu.Picha ya juu wakielekea gereza la keko baada ya masharti ya dhamana kuwa magumu.

Mambo ya KP

Huu ni mwanzo mzuri wadau kwa rangi yetu.Ni mfano mzuri wa kuigwa

TAKA

Nini kifanyike kwa hali kama hii?

BEDAJUNIOR: MWANZO MZURI KUKOMESHA UFISADI!

BEDAJUNIOR: MWANZO MZURI KUKOMESHA UFISADI!

MWANZO MZURI KUKOMESHA UFISADI!

Japo mwanzo ni mgumu lakini tunaamini kwa jitihada hizi,Mheshimiwa RAISI anawapa matumaini watanzania waliomchagua.Tunategemea jitihada hizi hazitoishia kwa BASIL MRAMBA na DANIEL YONA tu katika suala zima la kukomesha ufisadi bali kila anayestahili kufikishwa katika mkono wa sheria na ashughulikiwe.
Hii inawapa changamoto wananchi katika suala zima la maendeleo na imani katika serikali yao.Na tuone basi hizo hela zirudishwe,isiwe ikawa janja ya nyani.
bedajunior